Habari zenu ndugu watembeleaji wa blogu hii. Natumaini ni wazima wa afya na karibuni tena katika blogu hii. Leo nawalenga sana mabloga wenzangu na hata kama wewe pia utakuwa na ndoto za kuwa bloga basi hii inakuhusu.
Nimeona baadhi ya blogu zimefungia habari zake ili zisikopiwe na watu wengine ikiwa wao wamezikopy kutoka kwa bloga wengine. Wamezuia "text selection" na pia wameondoa "Lightclick function" lengo lao mtu asikopy habari yake. Kiukweli hii sio njia sahihi hata kidogo nikiwa bloga kama bloga napingana nayo na ni ngumu kuendelea kwa wewe ambaye umefunga habari zako zisikopiwe na bloga wengine.
Miongoni mwa njia nne za kuzuia mtu asikopy habari zako na kuziweka kwake zipo pia hizo za kuzuia "text selection" na "Remove rightclick funtion" Lakini kwa ulimwengu wa sasa sio nzuri sana kwani itakupotezea number of visitors katika blogu yako
Njia hizi hapa ndiyo nzuri sana kwa ulimwengu wa sasa njia hizo ni;
Water mark
DMCA
1.WATER MARK
Kiukweli kabisa njia hizi wewe kama bloga ndio njia nzuri za kuzitumia karne hii ya 21.Water mark inakusaidia kuongeza namba ya visitors yaani watembeleaji katika blogu yako au website.Hii watermark inawekwa katika picha za habari unazoziweka.Mfano mzuri tazama picha za "Millardayo "na " Global publisher" Hawa wanatumia water mark katika picha zao

.
Hiyo ni watermark ya Millardayo.com ambayo itamfanya apate watembeleaji wa kutosha katika website yake kwa yeyote atakaye ikopy ina kuwa ni rahisi kujua kwamba ameikopy kutoka kwa millard ayo hivyo siku nyingine ataenda moja kwa moja kwa millard lakini chanzo ni wewe kukopy habari yake.
Mfano mwingine huu hapa kutoka global publisher

Hiyo hapo ni water mark ya Global publisher ambayo itawatambulisha kwa yeyote atakaye kopy.
2.DMCA
Hapa katika DMCA Itakusaidia kukuongezea idadi ya page view kwa yeyote atakaye kopy habari yako. DMCA Hili ni kampuni la kuzuia duplicated content katika search engine kama google na nyinginezo.Kama wewe ni mvivu wa kuweka water mark basi tumia njia hii itakusaidia kwani Ukisha jiunga na huduma hii wao DMCA Watapokea message kutoka kwako kupitia e-mail yako.Ile habari yako ambayo imekopiwa, yule aliyekopy atapelekewa ujumbe kwamba search engine imegundua kuwa hii habari umeikopy kwa hiyo watembeleaji watakaoifungua katika blogu ya yule aliyekopy itaongeza page view kwako kawani inahesabika kama ya kwako.Mfano mzuri Blogu ya MALUNDE 1 BLOG Anatumia hii.
Kwa leo naomba tuishie hapa kama ukihitaji maelezo zaidi kuhusu DMCA Wasiliana nami kwa namba iliyopo katika bunner hapo juu kabisa mwanzoni
Wenu katika ulimwengu wa blog
Omary Mbaraka
Habari wapendwa leo nimeamua kuja na mada hii kutokana na sababu za msingi ikiwemo ya ongezeko la blogger wengi duniani kuongezeka kila siku. Watu wengi sasa wanamiliki blogu zaidi ya moja.Kama ni kweli basi somo hili litakusaidia kuongeza idadi ya watembeleaji katika blog yako.Kama una blogu zaidi ya moja basi blog moja weka hii widget katika blog yako.Usishangae hiyo widget ndio somo lenyewe tutakalojifunza.Hii itakusaidia kuongezeka kwa number ya page views katika blog yako.
Kama nilivyosema mwanzo kwamba hii widget kwa ajili ya blogger itakusaidia kuonyesha kiautomatiki zile post zako na picha katika hizo post kwa mvuto unaomvutia msomaji. Hii widget hupokea mabadiliko yenyewe kiautomatiki pale unapotuma post mpya na hauhitaji ku edit widget, picha,kichwa cha habari wala maelezo tena. Unachotakiwa ni kuweka codi za widget hii katika blog yako na utakuwa umemaliza kazi.
Jinsi ya kuweka kodi za widget hii katika blog .
Ili uweze kuweka fuata hatua hizi Nenda Blogger Dashbord→Add gadget→ HTML/Javascript. Baada ya hapo kopy kodi za hapa chini na uende ukazipaste hapo juu katika html/javascript.Ukisha paste kodi hizo bofya batani iliyoandikwa Save kisha malizia ku save mpangilio wa widget sehemu iliyoandikwa save arrangement. Ukimaliza ku save view blog yako na utaona hiyo widget inavyofanya kazi.
Kodi zenyewe za kukopi hizi hapa.
<link rel="stylesheet" type="text/css" href="http://blogger-json-experiment.googlecode.com/svn/resources/blogger-feed-rotator-plugin/default-style.min.css"/>
<div id="slider-rotator" class="slider-rotator loading"></div>
<script type="text/javascript" src="http://ajax.googleapis.com/ajax/libs/jquery/1.9.1/jquery.min.js"></script>
<script type="text/javascript" src="http://blogger-json-experiment.googlecode.com/svn/resources/blogger-feed-rotator-plugin/blogger-feed-rotator.min.js"></script>
<script type="text/javascript">
makeSlider({
url: "http://JINALABLOGYAKO.blogspot.com" // Add your blog URL
});
</script>
Kumbuka kutoa jina la blogyako na kuandika jina halisi la blog yako.
Ukiwa na tatizo toa maoni yako hapo chini. Siku njema wasomaji wangu tutaendelea kutoa mada tofautitofauti kupitia blog hii usisahau ku like page yetu ili upate habari zetu kwa urahisi.
Imeandaliwa na Omar Mbarak
Hapa ndio mahali husika katika kujifunza namna ya kuwa na blog yako na kuifanya iwe na mafanikio makubwa kama ambavyo wengine wamefanikiwa kupitia blog zao.
Kuna namna mbali mbali za kuwa na blog ila leo hapa nitazungumzia mbili tu ambazo ni rahisi sana. Kumbuka kuwa kuwa na blog yako mwenyewe hakuna gharama yoyote zaidi ya muda wako na ubunifu wako.
BLOGGER Kupitia uwanja huo au platform hiyo inayomilikiwa na Google unaweza kuanzisha blog yako mwenyewe ambayo itabebwa na jina ulipendalo wewe mfano:- http://blogyako.blogspot.com, hapo ambapo nimekoleza kwa maandishi ya rangi nyekundu ndipo ambapo utaweka jina la blog yako. Utaratibu mzima utaupata wakati ukiwa unaisajiri blog yako Bofya hapa ili kutengeneza blog yako Create a new Blog
WORDPRESS Hapa pia utaratibu ni kama hapo mwanzo ila hizi ni nyanja (Platforms) tofauti na zinatofautiana vikolombwezo (features) vya uboreshaji wa blogs. Hapa ukianzisha blog yako itabebwa na uwanja au platform ya wordpress. Namna ya jina la blog yako itakuwa katika mfano huu:- http://blogyako.wordpress.com. Ukitaka kuwa na blog kupitia wordpress tafadhali bofya hapa, Sign up For New Wordpress Naamini hadi sasa umeisha elewa namna ya kuweza kuanzisha blog yako, wakati mwingine nitazungumzia jinsi ya kuweza kuwa na blog yako ikiwa na domain yako mwenyewe mf:- www.domainyako.com kwa leo nisikuchoshe naishia hapa.
Imeandikwa na Omar Mbaraka
Subscribe to:
Posts (Atom)